Tuesday, October 16, 2007

Wana Atsa Juma Nyani(L)Kassim Mrefu(c) Salim Jumbe (L) wakipozi baada ya uchaguzi mkuu wa Atsa



Wana jumuia ya Atsa wakiwa pamoja na Mh Pr Peter Msola waziri wa elimu ya juu sayansi na teknolojia katika chuo kikuu cha Algers alipokutana na wanafunzi

Thursday, October 11, 2007

Wanafunzi wapya

Wanafunzi wapya wa fani mbali mbali kutoka Tanzaniawanatarajiwa kuwasili hapa Algeria siku ya tarehe 18/10/2007 saa 12:45 Mchana kwa shirika la ndege la Qatar airways.Wana jumuia nyote munaombwa mujiandae kuwapokea
Utaratibu kamili utatangazwa hapo baadae

CHAMA CHA WANAFUNZI WATANZANIA NCHINI ALGERIA

JINA NA HISTORIA YA CHAMA

a) Jina la chama ni : CHAMA CHA WANAFUNZI WATANZANIA NCHINI ALGERIA (Association of Tanzanian Students in Algeria) Kwa kifupi ATSA.

b)Chama kiliundwa na wanafunzi Watanzania wasomao nchini Algeria ; Mwezi Aprili mwaka 2002 katika mji mkuu wa Algeria, Algiers.

MLEZI WA CHAMA

Chama kina mlezi wake ambaye hupatikana kwa mapendekezo ya wanachama kwa wakati huo.

3.0. MALENGO YA CHAMA

Malengo na madhumuni makuu ya kuanzishwa chama ni pamoja na :

a)Kuwaunganisha wanafunzi Watanzania wote wasomao nchini Algeria katika kuwawezesha kuishi hali ya udugu, mshikamano na kujenga moyo thabiti wa kusaidiana na kushirikana.

b)Kubuni mbinu, mipango na mikakati mbalimbali na kuitekeleza kwa lengo la kuweka mazingira mazuri ya wanachama wake ili kupata maisha bora, na elimu iliyo nzuri.

AU

Kuandaa mazingira mazuri ya wanachama wake katika kuhakikisha wanapata maisha na elimu bora.

c)Kutafuta ufumbuzi, kushughulikia na kufuatilia matatizo makuu yanayowakabili wanachama wake hasa ya kiuchumi yanayotokana na gharama kubwa za kimaisha na kielimu.

d)Kutetea maslahi ya wanachama ikiwa ni pamoja na kusimamia kikamilifu na kuhakikisha wanapata haki zao zote kwa usawa na uadilifu bila upendeleo.

e)Kusimamia na kutekeleza kwa ujumla maazimio yote na maelekezo yatakayotolewa na wanachama.

f)Kudumisha uzalendo na kuendeleza uhusiano bora na jumuiya zingine za wanafunzi pamoja na mamlaka na ofisi mbalimbali hususani zile zinazoshughulikia masuala na matatizo ya wanafunzi.